Uliye na Mpango Wa Kuoa Unayatambua Haya??


Kwa wale ambao wanataka kuoa na kuolewa. hata wewe ambae umeoa na kuolewa inakuhusu.
Kwa nini unapingana na ndoa? Nafahamu unapingana na ndoa, lakini mimi bado nahitaji kuolewa. Kama unaweza nipe baraka zako.
Tafakari juu ya hilo. A fool and his cool are soon parted.
Hivyo ndivyo ndoa itakavyokuwa.  ni wasiojua tu hufikiria katika muda wa halali, vinginevyo, Upendo peke yake unatosha. Na mimi sipingani na ndoa– iam for love. kama mapenzi yamekuwa ndio ndoa, vizuri; lakini usitumaini kuwa ndoa italeta mapenzi. haiwezekani. Upendo unaweza kuwa ndoa. Unatakiwa ufanyie kazi ya ufahamu  kubadilisha  upendo kuwa ndoa.
Kuna hamu kubwa na matamanio ya  mapenzi, lakini upendo unahitaji ufahamu. na hapo tu inapofikia kwenye kilele cha juu– na hicho kilele ndio ndoa yenyewe. haiwezi kuingiliwa na sheria. ni mioyo miwili  imepatana na kupendana. ni kazi ya watu wawili– hio ndio ndoa.
Lakini watu wanajaribu upendo kwa sababu hawana ufahamu…Hamu yao ni nzuri, lakini  upendo huo umejaa wivu, kumilikiwa zaidi, kuwa na hasira zaidi, hapo ni haraka kuharibu uzuri wa ndoa.
Kwa miaka mingi ndoa zimekuwa  zinategemea  sheria ndio mlinzi wao endapo mtu ataharibu ndoa .Jamii, serikali, mahakama , polisi, wachungaji wote hawa watakulazimisha kuishi kwenye taasisi ya ndoa,  Na utakuwa kama mtumwa, kama ndoa yako ni ya taasisi,  Utaenda kuwa mtumwa wa taasisi.Ni watumwa tu ndio wanaishi kwenye hio.
Ndoa ni kitu tofauti sana: ila hatufahamu. Ni kilele cha mapenzi: ndio uzuri wenyewe.
Mimi sipingani na ndoa —Niko kwa ajili ya ndoa ya kweli. niko kinyume na uongo unaokuwepo. Lakini ni mpangilio. inakupa usalama, ulinzi, kazi na vingine. Inakupa ushirika, haikupi utajiri, haikupi ustawi.
Kwa hio kama unataka kuoa  kulingana na  ninavyosema mimi,  naweza kukupa baraka zangu.
Jifunze kupenda,  tupa kila kitu kilicho kinyume na upendo. ni kazi  ngumu,  ni sanaa ya kweli inatakiwa iwepo,  ili uweze kupenda. inahitaji  kuboreshwa, utamaduni wa ndani, utulivu,  ili mtu aweze kugundua kwa urahisi  na kuona haraka  ni nani anaelekea kuharibu
Kama utaepuka Uharibifu, kama utakuwa mbunifu kwenye mahusiano yako; kama utasaidia, kuboresha,sio tu hamu… hamu peke yake haiwezi kudumisha upendo. Huruma inahitajika . kama utaweza kuwa mwenye huruma kwa wengine; kama unaweza kukubali mapungufu yao, upeo wao; kama utaweza kumkubali jinsi alivyo na bado unampenda– kwa hio siku moja ndoa itatokea. inaweza kuchukua muda mrefu.  kitu ambacho kinaweza kuchukua maisha yako yote.
Unaweza kupata baraka zangu lakini  tofauti na hapo  hapana . hata hivyo baraka zangu hazikusaidii hata kidogo. Na uwe makini! Kabla hujarukia kwenye taasisi , Fikiria mara ya pili.
Uwe tu na angalau ufahamu kidogo. baraka zangu hazikusaidii. Ndoa ni kama mtego, ukiingia bila kufahamu utanaswa ushindwe kutoka.
Mama mmoja alikuwa anapenda sana kula supu ya kuku. Jioni moja  marafiki wa mume wake wakaja na taarifa kuwa mume wake amefariki kwa ajali. Wakati huo huyo mama alikuwa na bakuli lake la supu.  Hakuwaangalia wale watu. Aliendelea kunywa supu yake. wale watu wakamrudia tena kumwambia,  tazama , tunakuambia hivi mume wako amefariki!.Aligeuka kulia na kuwaambia kuwa , nitakapomaliza supu yangu  mtasikia nikipiga kelele.
Ndoa zinginethe  sio upendo. Ni kitu kingine.
Wema ni lugha ambayo kiziwi anaweza kusikia na kipofu anaweza kuona.
Kwa hio jitahidi uwe na angalau ufahamu kidogo kabla hujanaswa kwenye mtego. ndoa ni mtego. Ila usinifikirie vibaya nasema tu ninayoyafahamu. Unaweza ukategwa na mwanamke au ukamtega mwanamke. Ni mitego iliokomaa.  Na kwa hio  ya kisheria  mtakubaliana kuumizana maisha yenu yote. Hakuna talaka  hata kama mmoja atakufa.  mke mmoja mume mmoja mpaka mbinguni mtakapokutana tena.  Kumbuka hilo.
Usifanye haraka kuingia kwenye ndoa. Fikiria mara mbili kwanza kabla . Je unafahamu angalau kidogo?

Comments

Popular posts from this blog

10 Relationship Goals That Will Make Your Love Stronger

Katy Perry flashes her toned abs as she poses in a bright orange crop top with a matching skirt

Rebecca Klopper Video Viral On Twitter : Know everything about the viral video